ELIMU NI MUHIMU SANA :MAMA SALMA KIKWETE AWAASA WAALIMU NA WAZAZI KUWA SIMAMIA WATOTO VYEMA KATIKA ELIMU YAO - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


23 Apr 2014

ELIMU NI MUHIMU SANA :MAMA SALMA KIKWETE AWAASA WAALIMU NA WAZAZI KUWA SIMAMIA WATOTO VYEMA KATIKA ELIMU YAO

Na Anna Nkinda- Maelezo, Lindi
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi  (CCM) Taifa (NEC) wilaya ya Lindi mjini Mama Salma Kikwete amewataka wazazi na walimu kushirikiana kwa pamoja na kuhakikisha wanafunzi wanakwenda shule na kusoma  jambo ambalo litasaidia kupanda kwa kiwango cha elimu mkoani humo.

Mama Kikwete ambaye pia ni Mke wa Rais Jakaya Mrisho Kikwete alitoa rai hiyo hivi karibuni wakati akiongea na wananchi pamoja  na wanafunzi wa kijiji cha Ruaha waliofika kumsalimia mara baada ya kumaliza mkutano wake  na viongozi wa Halmashauri kuu ya tawi la Ruaha lililopo  katika kata ya Mingoyo  wilaya ya Lindi mjini.

Mjumbe huyo wa Halmashauri Kuu Taifa  alisema kiwango cha elimu katika mkoa huo kiko chini lakini kama wazazi watahakikisha watoto wao wanaenda shule kwa wakati na walimu wakihakikisha watoto wamefika shule na kuwafundisha kiwango cha elimu kitapanda kwa kiasi kikubwa.

“Na ninyi watoto muache tabia ya kupoteza muda kwa kuokota mabibo au maembe tumieni muda huo kusoma kwa bidii na kufanya vizuri katika masomo yenu kwa kufanya hivyo mtakuwa na maisha mazuri hapo baadaye”, alisema Mama Kikwete.

Akiwa katika matawi la Mkwaya, Ruaha na Majengo Mama Kikwete aliwataka vijana wa CCM kuungana kwa pamoja na  kutafuta eneo kubwa la kikundi ambalo watalitumia kulima  kilimo cha mazao ya biashara kama vile ufuta ambao utawapatia  fedha nyingi na hivyo kujikwamua kiuchumi.

Aidha Mama Kikwete pia aliwataka kinamama kwenda kupima saratani ya mlango wa kizazi ambayo inauwa wanake wengi lakini vifo vya ugonjwa huo vinazuilika kama mgonjwa atakwenda kupima mapema na akigundulika kuwa na dalili za ugonjwa huo katika hatua za awali ataweza kupata matibabu na kupona.

Mama Kikwete ambaye ni mjumbe wa NEC Taifa kupitia wilaya ya Lindi mjini alikutana na viongozi hao wa Halmashauri kuu ya tawi ya CCM kwa ajili ya kuimarisha kazi za chama hicho ikiwa ni pamoja na kufanya vikao na viongozi.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad