MICHEZO MATUKIO :PANONE FC ILIVYOPOKEA UGENI WA REAL MADRID KILIMANJARO - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


25 Aug 2014

MICHEZO MATUKIO :PANONE FC ILIVYOPOKEA UGENI WA REAL MADRID KILIMANJARO

Waziri wa Vijana,Utamaduni na Michezo Dk Fenera Mkangara akiongoza ugeni toka klabu ya Real Madrid ulipowasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA.)
Baadhi ya wachezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid wakiwasili katika uwanja wa Ndege wa KIA .
Mkurugenzi wa Kampuni ya Panone Ltd Patrick Ngiloi akisalimiana na mmoja wa wageni waliokuwa wameambatana na ugeni huo.
Magwiji hao walipokelewa na ngoma ya asili kutoka kikundi cha Msanja cha mjini Moshi.
Magwiji hao walikabidhiwa Maua uwanjani hapo kama ishara ya Upendo kwao 

Mkurugenzi wa Panone Ltd,Patrick Ngiloi (kushoto) akiteta jambo na Mkurugenzi wa TSN ,FarouK Baghoza mara baada ya kupokea ugeni toka Real Madrid.
Ugeni wa Real Madrid ukiwasili katika hotel ya Panone Luxury Motel iliyopo King'ori jijini Arusha.
Waziri wa Habari ,Vijana ,Utamaduni na  Michezo Dk Fenela Mkangara akiongozana na mkuu wa wilaya ya Rombo ,Elinasi Parangyo kusindikiza Ugeni toka Real Madrid.
Wachezaji wa Real Madrid wakiteremka toka katika basi wakiingia hotel ya Panone Luxury Motel kwa jaili ya viburudisho.
Viongozi wa serikali wakipata viburudisho
Baadhi ya wachezaji wa klabu ya Panone fc wakibadilishana mawazo na baadhi ya wachezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid .
Wadau wa soka mkoa wa Kilimanjaro pia walikuwepo.
Wachezaji wa klabu ya Panone fc ,Raymond Madesho (shoto) na Salmini Mvungi wakipata picha ya pamoja na mtangazaji wa Clouds fm Shaffih Dauda.
Mkurugenzi wa kampuni ya Panone Ltd ,Patrick Ngiloi akikabidhi zawadi ya kinyago kwa Waziri wa Habari,Vijana ,Utamaduni na Michezo Dk Fenela Mkangara ,kulia ni mkurugenzi wa kampuni ya Ibra line,Ibrahim Shayo.
Waziri wa Habari,Vijana ,Utamaduni na Michezo Dk Fenela Mkangara akikabidhi zawadi ya kinyago kwa Kiongozi wa Wachezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid.
Waziri wa Habari,Vijana ,Utamaduni na Michezo Dk Fenela Mkangara akizungumza mara baada ya kukabidhi zawadi kwa wageni hao. 
Baaadhi ya wageni wakiwa na wenyeji wao katika hotel ya Panone Luxury Motel.
Waziri Mkangara akiongoza ugeni kutoka hotelini hapo.
Kikosi cha wachezaji wa zamani waklabu ya Real Madrid kikiasili katika uwanja wa Ushirika.
Kikosi cha Machava fc .
Kikosi cha Panone fc.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama akiwapokea wageni hao.
Wageni wakijiandaa kusalimia vikosi vya Panone fc na Machava fc.
Kikosi cha Machava wakiwa katika picha ya Pamoja na magwiji wa Real Madrid.
Kikosi cha Panone fc kikiwa katika picha ya pamoja na magwiji wa Real Madrid.
Friends Of Panone wakiwa katika picha ya Pamoja na magwiji hao.
Picha na Dixon Busagaga

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad