MIPAKA YETU :RAIS JAKAYA KIKWETE KUZINDUA PROGRAMU YA UIMARISHAJI WA MIPAKA YA KIMATAIFA MKOANI KAGERA. - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


26 Aug 2014

MIPAKA YETU :RAIS JAKAYA KIKWETE KUZINDUA PROGRAMU YA UIMARISHAJI WA MIPAKA YA KIMATAIFA MKOANI KAGERA.


 Kaimu Katibu Tawala wa wilaya ya Ngara Bw. Hussein Seif akitoa ufafanuzi kwa wajumbe wa maandalizi ya shughuli ya uzinduzi wa Programu ya uimarishaji wa mipaka ya Kimataifa wa wilaya ya Ngara itakayozinduliwa na Rais Jakaya Kikwete eneo la Mugikomero mpakani mwa Tanzania na Burundi. Wanaoonekana nyuma ni raia wa Burundi waishio mpakani.
Raia wa Burundi wakiwa nyuma ya alama ya mpaka inayotenganisha Tanzania na Burundi. Serikali kupitia Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi inaendelea na zoezi la kuhuisha mipaka hiyo ya kimataifa.
*************************************
Na. Aron Msigwa – MAELEZO Ngara, Kagera.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Kikwete anatarajia kuwa mgeni rasmi katika  uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa kwa lengo la kuhuisha alama zilizopo na kuweka mpya katika maeneo ya  mipaka ya Tanzania ambayo awali yalikuwa yametengwa na mito na baadaye mito hiyo kukauka .
Programu hiyo inayofanywa na wataalam wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi itazinduliwa rasmi Agosti 28, katika eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare  kwa upande wa Burundi.
 Aidha, itahusisha ujenzi na uwekaji wa vigingi vya mipaka, Marais wa nchi za Burundi na Tanzania kutembelea baadhi ya maeneo yenye alama za mipaka na kisha kuzungumza na wananchi waishio mpakani.
Katika tukio hilo Rais Jakaya Kikwete anatarajia kumpokea mwenzake wa Burundi, Rais Pierre Nkurunziza atakayewasili nchini Tanzania kushuhudia zoezi hilo akitokea nchini Burundi kupitia mpaka wa Kabanga ulioko wilayani Ngara.
Kaimu Katibu Tawala wa wilaya ya Ngara Bw. Hussein Seif akizungumzia maandalizi ya shughuli hiyo amesema kuwa wilaya hiyo imejipanga kuhakikisha kuwa programu hiyo inatekelezwa kwa ufanisi katika maeneo yote ya wilaya ya Ngara yanayopakana na nchi ya Burundi.
Naye Mkurugenzi Msaidizi wa Topographia na Giodosia wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. James Mtamakaya akizungumzia zoezi hilo amesema kuwa tayari maeneo mbalimbali ya mipaka ya Tanzania yameshapitiwa na zoezi hilo likiwemo eneo la mpaka kati ya Tanzania na Uganda.
Ameyataja maeneo mengine kuwa ni eneo la Tanzania na Rwanda ambalo bado linatenganishwa na mto Rusumo, eneo la mpaka kati ya Tanzania na Msumbiji, Tanzania na Kenya pamoja na zoezi la uimarishaji wa mpaka kati ya Burundi na Tanzania ambalo linaendelea kufanyika.
Dkt.Mtamakaya ameeleza kuwa zoezi hilo lina umuhimu katika kuhakikisha ulinzi na usalama wa mipaka  na kuongeza kuwa ni utekelezaji wa azimio la Umoja wa Afrika (AU) kwa nchi wanachama kuhakikisha kuwa ifikapo mwaka 2017 kila nchi iwe imekamilisha programu hiyo.
Akizungumzia changamoto wanazokutana nazo wakati wa uendeshaji wa zoezi hilo amesema ni pamoja na uelewa mdogo wa wananchi hususani raia wa pande zote ambao wengi wao wamejenga ndani ya maeneo ya hifadhi ya alama za mipaka ambayo kisheria hayaruhusiwi kujengwa kutokana na alama za mipaka zilizowekwa na wakoloni kuwa umbali mrefu kutoka eneo moja hadi jingine.
“Baada ya kuanza kwa zoezi la kuhuisha mipaka baadhi ya Raia wa Tanzania na Burundi wamejikuta wamejenga  ndani ya eneo la mpaka ambalo haliruhusiwi  jambo  kinyume cha sheria za kimataifa, wengi wao wamejenga  kwenye maeneo hayo kwa kuvamia kutokana na mipaka iliyowekwa na wakaoloni kuwa umbari mrefu nao kujikuta wamo eneo la nchi nyingine lazima taratibu za kuwaondoa zifanyike ” Amesisitiza Dkt. Mtamakaya.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad