UCHUMI WETU :RAIS JAKAYA KIKWETE ATAKA MSAADA ESRF KUONDOA UMASKINI KWENYE UCHUMI UNAOKUA KWA KASI KUBWA - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


12 Sept 2014

UCHUMI WETU :RAIS JAKAYA KIKWETE ATAKA MSAADA ESRF KUONDOA UMASKINI KWENYE UCHUMI UNAOKUA KWA KASI KUBWA

DSC_0389
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akifungua rasmi mkutano mkubwa wa tatu wa ESRF unaozungumzia ukuaji wa uchumi kwa kutumia fursa zilizopo na maendeleo yanayogusa jamii uliofanyika jana jijini Dar katika hoteli ya Hyatt Regency, Kilimanjaro.
DSC_0039
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi Huru ya Utafiti wa Uchumi na Jamii (ESRF), Dk. Hoseana Lunogelo akisalimiana na Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini , Alvaro Rodriguez nje ya ukumbi wa mikutano kabla ya mgeni rasmi kuwasili kwenye mkutano mkubwa wa tatu wa ESRF unaozungumzia ukuaji wa uchumi kwa kutumia fursa zilizopo na maendeleo yanayogusa jamii uliofanyika jana jijini Dar katika hoteli ya Hyatt Regency, Kilimanjaro. Picha na Zainul Mzige
DSC_0039
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi Huru ya Utafiti wa Uchumi na Jamii (ESRF), Dk. Hoseana Lunogelo akisalimiana na Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini , Alvaro Rodriguez nje ya ukumbi wa mikutano kabla ya mgeni rasmi kuwasili kwenye mkutano mkubwa wa tatu wa ESRF unaozungumzia ukuaji wa uchumi kwa kutumia fursa zilizopo na maendeleo yanayogusa jamii uliofanyika jana jijini Dar katika hoteli ya Hyatt Regency, Kilimanjaro. Picha zote na Zainul Mzige
 
DSC_0349
DSC_0455
Mkurugenzi wa Programu wa ESRF ambaye pia ni Mratibu wa Mradi wa taarifa ya maendeleo ya watu nchini Tanzania (THDR), Dr. Tausi Kida akifuatilia kwa makini hotuba ya mgeni rasmi (hayupo pichani) wakati wa mkutano huo.
DSC_0393
Mjumbe wa Bodi ya wadhamini ESRF, Prof. Sylvia Temu akitoa neno la shukrani kwa mgeni rasmi.
DSC_0444
Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akizungumza kwa niaba ya Umoja wa Mataifa wakati wa mkutano huo. Kulia ni Gelase Mutahaba kutoka Chuo kikuu cha Dar es Salaam, Kushoto ni Prof. Bertil Tungodden kutoka nchini Norway na Mjumbe wa Bodi ya wadhamini ESRF, Prof. Sylvia Temu (wa pili kushoto).
DSC_0257
Pichani juu na chini ni Baadhi ya wawakilishi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini, mabalozi, taasisi mbalimbali za serikali waliohudhuria mkutano huo uliofanyika kwenye hoteli ya Hyatt Regency, Kilimanjaro jijini Dar.
DSC_0265
DSC_0259
DSC_0267

*SEKTA ZA MADINI ,UMEME NA KILIMO ZAKUZA PATO LA TAIFA.

Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Bw. Morrice Oyuke (katikati) akizungumza  na waandishi wa habari kuhusu ukuaji wa Pato la Taifa kwa bei ya Soko leo jijini Dar es salaam. Wengine ni Bw. Oswald Ruboha (kulia) Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Sera na Mipango, Wizara ya Kilimo na Dkt. Stephen Kirama (kushoto), Mhadhiri wa Uchumi, Chuo Kikuu cha Dar es salaam.
Na. Aron Msigwa – MAELEZO
Sekta ya Kilimo,Uvuvi,  Viwanda , Nishati na Madini zimeelezwa kuwa miongoni mwa sekta muhimu zinazoongoza zaidi katika kuchangia kukua kwa pato la Taifa hadi asilimia 7.4 katika robo ya kwanza ya mwaka 2014.
Kwa mujibu wa taarifa zilizokusanywa kutoka katika vyanzo mbalimbali vya uzalishaji nchini na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) kwa kutumia kanuni za kimataifa kukokotoa pato la Taifa zinaonyesha kuwa sekta hizo zimetoa mchango mkubwa wa kukua kwa pato la Taifa  kwa asilimia 7.4 kuanzia mwezi Januari hadi  Machi, 2014 ikilinganishwa na asilimia 7.1 za mwaka 2013.

Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Bw. Morrice Oyuke akizungumzia ukuaji wa Pato la Taifa kwa bei ya Soko leo jijini Dar es salaam amesema kuwa Pato la Taifa katika robo ya mwaka 2014 kuanzia Januari hadi Machi limekua kwa asilimia 7.4 kutokana na kukua kwa sekta za Kilimo, Uvuvi, Viwanda, Ujenzi, Umeme na  utoaji wa huduma.

Amesema sekta zilizofanya vizuri katika ukuaji huo ni pamoja na sekta ya uchimbaji wa Madini, mawe na kokoto ambayo imekua kwa asilimia 8.7 ikilinganishwa na asilimia 1.7 za mwaka uliopita kutokana na kukua kwa masoko ya uuzaji ya nje ya nchi. 
Ameongeza kuwa sekta uzalishaji wa bidhaa za viwandani imekua kwa asilimia 8.5 kutoka 8.3 huku shughuli za utoaji wa huduma na uchumi zikiwemo za ukarabati wa magari, pikipiki na vifaa vingine vya majumbani zikikua kwa asilimia 8.0 kwa robo ya mwaka 2014.
Bw. Oyuke ameeleza kuwa shughuli za uchukuzi na mawasiliano zimefikia kasi ya ukuaji wa asilimia 16.5 katika kipindi hicho na kuongeza kuwa huduma za hoteli na migahawa zimefikia kasi ya ukuaji wa asilimia 3.0, huku shughuli za uendeshaji wa Serikali zikifikia asilimia 5.1, Elimu asilimia 5.2, huduma za Sfya na  shughuli nyingine zikikua kwa asilimia 4.5.
Aidha, amefafanua kuwa sekta ya umeme katika robo ya mwaka 2014 imekua kwa asilimia 12.6 ikilinganishwa na asilimia 6 ya mwaka uliopita kutokana na kupatikana kwa vyanzo mbadala vya kuzalisha umeme hususan ugunduzi wa gesi nchini ambao umeondoa tatizo la utegemezi wa umeme wa maji katika kuzalisha umeme.
“Kwa kipindi kirefu sekta ya umeme imekuwa na mawimbi kwa kiasi kikubwa , umeme wetu umekuwa wa kutegemea maji ya mvua, baada ya juhudi za Serikali na kugundulika kwa nishati ya Gesi nchini na kupatikana chanzo mbadala cha nishati tatizo hili limeshghulikiwa sasa sekta hii imeimarika” Amesisitiza.
Amesema Tanzania sasa inafanya vizuri kiuchumi katika nchi za Afrika ya Mashariki kwa kuwa ya pili ikifuatiwa na Uganda, Rwanda na Burundi na kuongeza kuwa hali ya amani na utulivu iliyopo nchini inaiweka Tanzania katika nafasi nzuri ya kukua zaidi kiuchumi.
Kwa upande wake mtaalam wa wa Uchumi kutoka Benki Kuu ya Taifa (BOT) Bw. Davidi Kwimbere akifafanua kuhusu hali iliyopo ya ukuaji wa uchumi amesema kuwa imechangiwa na kuongezeka kwa shughuli za uzalishaji .
Amesema sekta ya Kilimo na uzalishaji wa mazao imekua kutokana na matumizi ya mbolea, zana bora za kilimo, mbegu bora, madawa na kufafanua kuwa endapo juhudi zaidi zitaendelea kufanywa na wananchi kwa kuingia katika shughuli mbalimbali za uzalishaji uchumi utaendendelea kuonekana kwa mtu mmoja mmoja.
Amefafanua kuwa maendeleo katika nchi yoyote  yanachukua muda na kutoa wito kwa nchi za Afrika kuendelea kujifunza  na kufafanua kuwa nchi zote zilizopiga hatua kimaendeleo mpaka kufikia asilimia 15 ikiwemo China iliwachukua miaka 20 kuondoa umasikini. 
Amesema Tanzania inayo nafasi nzuri kukua kiuchumi kutokana na kuendelea kuimarika kwa miundombinu  na ukuaji wa sekta za ujenzi, Nishati, madini, Viwanda, umeme , kilimo na uvuvi hali inayochangia kuongezeka kwa uwekezaji.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad