MAISHA YETU :MKUTANO WA MABADILIKO YA TABIANCHI, UHAKIKA WA CHAKULA NA HAKI ZA ARDHI WAFANYIKA ,JIJINI DAR - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


1 Oct 2014

MAISHA YETU :MKUTANO WA MABADILIKO YA TABIANCHI, UHAKIKA WA CHAKULA NA HAKI ZA ARDHI WAFANYIKA ,JIJINI DAR


Robert Muthami Program Support Officer kutoka Pan African Climate Justice Alliance (PACJA) akitoa ufafanuzi juu ya baadhi ya mambo yanayohusu mabadiliko ya Tabianchi.
Kulia ni mmoja wa walalamikaji kutoka Loliondo akielezea kwa uchungu jinsi Muwekezaji alivyo wanyang'anya Ardhi yao na mpaka sasa hakuna kitu ambacho kinaendelea na wanahitaji kupata Msaada wa kisheria ili wapate rudishiwa Ardhi yao.
 Kulia ni Mama kutoka Loliondo akitoa malalamiko yake Mbele ya Mahakama ya wazi Jinsi mwekezaji alivyochukua Ardhi, kusababisha uharibifu na akina mama kuteseka pamoja na wengine kuharibu Mimba zao pia kupoteza watoto ambapo mpaka sasa kuna mtoto hajaonekana.
 Mlalamikaji Mwingine kutoka Loliondo akielezea Mbele ya Mahakama ya wazi  jinsi ya eneo lao lilivyochukulia na mwekezaji, na kutaka agizo la Mh. Waziri Mkuu lifanyiwe kazi la kwamba ardhi ile ni ya wafugaji na wanatakiwa warudishiwe
Mmoja wa walalamikaji kutoka Wilaya ya Kishapu akitoa malalamiko yake mbele ya Mahakama ya wazi juu ya walivyo chukuliwa maeneo kwa ahadi ya kuyaendeleza na kuto fanya hivyo, na kuomba eneo hilo ambalo ni mashamba warudishiwe ili waendelee na kilimo kwa kuwa eneo hilo kuna shida ya njaa.
Mchangiaji kutoka Oxfam Bwana Marc akizungumza juu ya haki za binadamu na moja ya haki hizo ni haki ya kila mwanadamu kuwa na Chakula, na kuongezea kuwa hata Umoja wa Mataifa unafahamu hilo Pia amesisitiza kuwa ni jukumu la kila mtu kujua sheria za umiliki wa Ardhi
Mjumbe wa Bodi kutoka Forum CC akizungumza jambo wakati wa Mkutano huo
Mh. Jaji Richard Mziray Akitoa Maelezo ya kina juu ya Walalamikaji kutoka Loliondo ambao walikuwa wana malalamiko ya Ardhi na Kishapu ambapo walikuwa wanataka Eneo lao lirudishwe, Ametoa maelekezo ya yale ambayo wanatakiwa wayafuate.

 

Washiriki wa Mkutano huo
 Mama Shujaa wa Chakula 2014 akichangia maada
 Burudani Elimisha ikiendelea
 Wadau wameguswa na kujumuika kucheza
 Picha ya pamoja

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad