SIASA ZETU :MSAFARA WA KINANA WASAFIRI KWA BAISKELI MILIMA YA USAMBARA KWENDA MKINGA,TANGA - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


1 Oct 2014

SIASA ZETU :MSAFARA WA KINANA WASAFIRI KWA BAISKELI MILIMA YA USAMBARA KWENDA MKINGA,TANGA

 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiwa na viongozi, waandishi wa habari pamoja na wananchi wakiendesha baiskeli kwenda Kata ya Mg'aro katika mteremko wa milima ya Usambara, akitokea Lushoto kwenda Wilaya ya Mkinga,  mkoani Tanga jana kuendelea na ziara ya kuimarisha uhai wa chama, kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM pamoja na kusikiliza kero za wananchi na kutafutia ufumbuzi.
Kinana na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye wakiongoza msafara katika safu ya milima ya Usambara kwenda Jimbo la Mkinga, Tanga.
Nyuma ya Nape ni Mkuu wa Wilaya ya Lushoto, Majid Mmanga na nyuma ya Kinana ni Mhariri wa Habari wa gazeti la Jambo Leo, Said Mwishehe.
Ni safari ndefu lakini yenye faraja na matumaini
Mbele ni Kinana na Mwandishi wa Habari Mwandamizi wa gazeti la Uhuru, Seleman Jongo .
Nape akiwasili katika Kata ya Mg'aro mpakani mwa Wilaya ya Lushoto na Mkinga. Pia Kata hiyo inapakana na Kenya.
Kinana na Nape wakifuahi baada ya kuwasili salama baada ya kutumia usafiri wa baiskeli
Wanahabari waliosafiri kwa baiskeli wakipumzika baada ya kufika katika Kata ya Mg'aro
Nape akihutubia wananchi katika Kata ya Mg'aro mpakani mwa wilaya za Lushoto na Mkinga
Watoto wakiwa juu ya kisiki cha mti wakiwa na hamu ya kumuona Katibu Mkuu wa CCM, Kinana akihutubia katika Kata ya Mg'aro.
Kinana akihutubia katika Kijiji cha Mg'aro ambapo aliwahakikishia wananchi wa eneo hilo kuwa barabara ya kutoka Lushoto kwenda Mkinga itaboreshwa, halafu na umeme utawekwa katika Kata hiyo.
Kinana akiagana na Mkuu wa Wilaya ya Lushoto baada ya msafara wake kukabidhiwa kwa uongozi wa Wilaya ya Mkinga katika Kata ya Daluni.
Kinana akiangalia ngoma ya utamaduni iliyokuwa ikitumbuiza wakati wa mapokezi katika Kijiji cha Daluni, wilayani Mkinga.
Kinana akishiriki ujenzi wa jengo la Zahanati katika Kijiji cha Daluni, wilayani Mkinga.
Kinana akisalimiana na wananchi baada ya kuwasili katika Kata ya Maramba.
Kinana akishiriki ujenzi wa jengo la Kituo cha Polisi Maramba.PICHA ZOTE NA KAMANDA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad