UTALII NA MATUKIO :WIZARA YA MALIASILI YABARIKI KUANZISHWA KWA MFUKO WA KULINDA MLIMA KILIMANJARO NA MLIMA MERU - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


24 Oct 2014

UTALII NA MATUKIO :WIZARA YA MALIASILI YABARIKI KUANZISHWA KWA MFUKO WA KULINDA MLIMA KILIMANJARO NA MLIMA MERU


Waziri wa Maliasili na Utalii,Lazaro Nyalandu akizungumza wakati wa kikao kilicho shirikisha Kamati ya Bunge ya Ardhi,Maliasili na Mazingira,Wabunge katika majimbo ya mikoa ya Arusha na Kilimanjaro,Wakuu wa wilaya zinazopakana na mlima Kilimanjaro na mlima Meru,TANAPA na Idara ya Misitu,(kulia)ni kaimu mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro ,Ibrahim Msengi.
Naibu waziri wa TAMISEMI ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Siha ,akichangia wakati wa kikao cha kuanzishwa kwa mchakato wa uanzishwaji mfumo wa kiikolojia wa mlima Kilimanjaro na Mlima Meru ambao utalinda milima yote miwili.
Makamau mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Ardhi,Maliasili na Mazingira,Abdulkarim Shah akizungumza katika kikao hicho kimetokana na wabunge wa mkoa wa Kilimanjaro kuomba kuanzishwa kwa mfuko wa kulinda mlima Kilimanjaro.
Baadhi ya washiriki wa kikao hicho kilichofanyika katika Hotel ya Sal salnero wakifuatilia michango mbalimbali iliyokuwa ikitolewa katika kikao hicho.
Mbunge wa Jimbo la Vunjo ,Agustino Mrema akichangia hoja katika kikao hicho.
Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki ,Joshua Nassar akichangia katika uanzishwaji wa mfuko huo.
Katibu wa Mbunge wa Moshi mjini,Basil Lema akichangia jambo katika kikao hicho akiwa amemwakilisha Mbunge Philemoni Ndesamburo.
Baadhi ya washiriki katika kikao hicho.
Kaimu mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya Moshi Ibrahimu Msengi akichangia katika uanzishwaji wa mfuko wa kulinda mlima Kilimanjaro na mlima Meru.
Mkuu wa wilaya ya Rombo Elinasi Palangyo akizungumza katika kikao hicho,wilaya ya Rombo ni moja ya wilaya ambazo zinapakana na mlima Kilimanjaro.
Mkuu wa wilaya ya Siha Dk ,Charles Mlingwa akizungumza katika kikao hicho,wilaya ya Siha ni moja ya wilaya ambazo zinapakana na mlima Kilimanjaro.
Mkuu wa wilaya ya Hai,Novatus Makunga akizungumza katika kikao hicho,wilaya ya Hai ni moja ya wilaya ambazo zinapakana na mlima Kilimanjaro.
Mbunge wa Arumeru Mashariki ,Joshua Nassar,akiwa pamoja na Mbunge Suzan Kiwanga na katibu wa Mbunge wa jimbo la Moshi mjini ,Basil Lema.
Mkurugenzi wa Wakala wa Misitu (TFS) Juma Mgoo akieleza namna ambavyo mfuko huo utasaidia katika kuimarisha ulinzi wa rasilimali ya misitu.
Mhifadhi mkuu wa hifadhi ya Arusha(ANAPA) Betrita Loibook akichangia katika kikao hicho.
Mhifadhi ,idara ya ujirani mwema ,Theodora Batiho akichangia jambo katika kikao hicho.
Washiriki wa kikao hicho wakifuatilia majadiliano.
Waziri wa Maliasili na Utalii,Lazaro Nyalandu akihitimisha kikao cha majadiliano juu ya kuanzishwa kwa mfuko wa kulinda mlima Kilimanjaro na Mlima Meru.
Na Dixon Busagaga

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad