Mfungaji
wa bao pekee la Simba dhidi ya Ruvu Shooting, Emmanuel Okwi
akishangilia wakati wa mchezo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara
uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Taifa.
Wachezaji wa Simba wakishangilia baada ya Okwi kuifungia timu yake bao pekee.
Mshambuliaji wa Simba, Emmanuel Okwi akiwatoka mabeki wa Ruvu Shooting.
Mchezaji wa Ruvu Shooting, Abdulrahman Musa (kulia) akiwania mpira na Elius Maguli wa Simba.
Kocha wa Simba, Patrick Phiri akikumbatiana na Okwi baada ya mchezo na tmu yake kupata ushindi wa kwanza tangu kuanza kwa Ligi.
Wachezaji wa Simba wakishangilia ushindi wa timu yao baada
ya kuifunga Ruvu Shooting 1-0 katika mchezo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara
uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Okwi akiwa na furaha baada ya kuifungia timu yake bao pekee.
Mashabiki wa Simba wakiwa na furahi. Picha na Francis Dande
No comments:
Post a Comment