Matukio :Mhadhiri wa Chuo Kikuu Mzumbe Awataka Maafisa Ugavi na Manunuzi nchini Kuzingatia Ubora na Viwango - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


24 Feb 2015

Matukio :Mhadhiri wa Chuo Kikuu Mzumbe Awataka Maafisa Ugavi na Manunuzi nchini Kuzingatia Ubora na Viwango


TA1
Afisa Mwandamizi Uraghibishi wa Ushindani,Alex Mbaga akizungumza kwenye semina hiyo leo kwa wataalamu wa manunuzi na ugavi kutoka taasisi mbalimbali juu ya manunuzi yanayozingatia thamani (Value for Money) iliyofanyika kwenye hotel ya Tanga Beach Resort mjini hapa.
TA2
Mkuu wa Idara ya Cartels (Makubaliano yanayodhirisha ushindani) kutoka Tume ya Ushindani Dar es Salaam,Shedrack Nkelebe akisisitiza jambo kwenye semina hiyo iliyohusisha wataalamu wa manunuzi na ugavi kutoka taasisi mbalimbali juu ya manunuzi yanayozingatia thamani (Value for Money) iliyofanyika kwenye hotel ya Tanga Beach Resort mjini hapa.
TA3
wataalamu wa manunuzi na ugavi kutoka taasisi mbalimbali nchini wakifuatilia semina ya juu ya manunuzi yanayozingatia thamani (Value for Money) iliyofanyika kwenye hotel ya Tanga Beach Resort mjini hapa
TA4
Wataalamu wa manunuzi na ugavi kutoka taasisi mbalimbali nchini wakifuatilia semina ya juu ya manunuzi yanayozingatia thamani (Value for Money) iliyofanyika kwenye hotel ya Tanga Beach Resort mjini hapa
TA5
Washiriki wa semina hiyo wakiwa kwenye picha ya pamoja leo iliyofanyika kwenye hotel ya Tanga Beach Resort mjini hapa
TA6
Washiriki wa semina hiyo wakiwa kwenye picha ya pamoja leo iliyofanyika kwenye hotel ya Tanga Beach Resort mjini hapa
TA7
Bi Martha Mapalala kutoka mmoja wa waratibu wa semina hiyo inayofanyika mkoani Tanga.
...................................................................................
NA MWANDISHI WETU,TANGA MAAFISA Ugavi nchini wametakiwa kuzingatia ubora wa vitu vinavyonunuliwa kwenye maeneo yao jambo ambalo litapelekea kuondoka bidhaa feki kwenye soko.

Wito huo ulitolewa leo na Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Mzumbe, Noel Mrope wakati wa semina ya wataalamu wa manunuzi na ugavi kutoka taasisi mbalimbali juu ya manunuzi yanayozingatia thamani (Value for Money) iliyofanyika kwenye hotel ya Tanga Beach Resort mjini hapa.

Semina hiyo ilikuwa na lengo la kuwajengea uwezo maafisa hao juu ya umuhimu wa kufanya manunuzi yanayozingatia thamani halisi ya fedha iliyoendeshwa na bodi ya taaluma ya manunuzi na ugavi nchini (PSPTB).

“Pamoja na kuzingatia sheria za Manunuzi lakini kwa kinachonunuliwa kuanzia fedha zilizotumika kwenye manunuzi kwa sababu hali hii itawezesha kuondoa uwepo wa bidhaa feki zinazosambazwa kwenye masoko “Alisema Mdhahiri huyo.

Aidha alisema kuwa mambo ya muhimu yaliyotiliwa mkazo kwenye semina hiyo ni namna ya wataalamu hao kuangalia thamani ya kitu na jinsi gani kinaweza kutumika katika kupandisha thamani yake na ubora ili mwisho wa siku watu wengi waweze kukitumia kitu hicho. “Katika jambo hili lazima wataalamu wa manunuzi kuhakikisha kwa pamoja wanafuata taratibu za manunuzi kwa kuzingatia sheria lengo likiwa kuona uthamani na ubora wa kitu ikiwemo thamani ya fedha halisi iliyotumika “Alisema.

Alisema kuwa kuwa kimsingi maafisa hayo wanatakiwa wanapokwenda kununua vitu wasikimbilie bei ya chini bali waangalie ubora na thamani ya kitu halisia ili kuweza kuzipa changamoto bidhaa zisizokuwa na kiwango kukosa soka na hatimaye kuondoka kwenye soko la ushindani.

Hata hiyo alisema kuwa wananchi wanapobaini kuna vitu vimefanyika kwenye Halmashauri yao chini ya kiwango wanapaswa kulalamika kupitia maeneo husika ili kuweza kukabiliana na hali hiyo.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad