Siasa Zetu : Mhe. Edward Lowassa Azidi Kujipatia Wadhamini Mkoani Manyara - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


26 Jun 2015

Siasa Zetu : Mhe. Edward Lowassa Azidi Kujipatia Wadhamini Mkoani Manyara

Msafara wa Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa ukipokelewa kwa shangwe na wanaCCM na Wananchi wa Mji wa Babati, Mkoani Manyara, wakati alipowasili kwenye mji huo kusaka wadhamini  watakaomuwezesha kutapa ridhaa ya chama chake kuwania Urais wa Tanzania kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, 2015. PICHA ZOTE NA OTHMAN MICHUZI.
Sehemu ya Wakazi wa Mji wa Babati wakimshangilia Mh. Lowassa pale walipomuona.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa na baadhi la viongozi wa CCM Mkoa wa Manyara wakati alipowasili kwenye Ofisi Kuu za Chama hicho, Mjini Babati Juni 25, 2015.
 
Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa akimsalimia Kijana Jacob Jeremiah ambaye ni mlemavu wa miguu, alipokutana nae nje ya Ofisi Kuu ya CCM Mkoa wa Manyara, iliopo Mjini Babari leo Juni 25, 2015, wakati akiwa katika ziara ya kusaka wadhamini  watakaomuwezesha kutapa ridhaa ya chama chake kuwania Urais wa Tanzania kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, 2015.

Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa (wa pili kulia), Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Arusha,Onesmo Ole Nangole pamoja na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa, Jesca Msambatavangu wakitembea sambamba na wanaCCM wengine kuelekea kwenye uwanja wa CCM Wilaya ya Babati, tayari kwenda kukabidhiwa fomu za Wadhamini, leo Juni 25, 2015.
Mh. Lowassa akisaini kutabu cha Wageni cha Ofisi ya CCM Wilaya ya Babati, Mkoani Manyara.
Muimbaji wa Nyimbo za Injili, Bahati Bukuku akiimba moja ya nyimbo zake wakati akiwasalimia WanaCCM na Wananchi wa Mji wa Babati, Mkoani Manyara Juni 25, 2015.
Sehemu ya WanaCCM na Wananchi wakazi wa Mji wa Babati Mkoani Manyara, wakiwa kwenye Uwanja wa CCM Wilaya ya Babati.
Mjumbe wa NEC kutoka Wilaya ya Mlele, Mkoani Katavi, Kampala Thomas Maganga akiwasalimia wanaCCM wa Mji wa Babati Mkoani Manyara.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa, Jesca Msambatavangu akisema neno wakati akiwasalimia wanaCCM na Wananchi wa Mji wa Babati, Mkoani Manyara leo Juni 25, 2015.
Mbunge wa Jimbo la Babati Mjini, Mh. Kiseryi Chambiri akizungumza jambo wakati Mh. Lowassa alipofika kuomba udhanini wa WanaCCM wa Mji wa Babati, Mkoani Manyara Juni 25, 2015.
Meza kuu.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad